Saturday, June 30, 2012

MCHUNGAJI BURTON SANGA ANAKUKARIBISHA KATIKA BLOG YAKE MPYA AMBAYO ITAKUWA INATOA HABARI ZA MUNGU NA MIKUTANO YAKE. KARIBUNI SANA WAPENDWA








WE ARE BUILT WITH THE WORD

Wise Man Harry gave an inspiring message to launch the service, titled, “Love Everyone, Trust Only God”.  He said that one of the great lessons life itself teaches us is that trust should not be readily given because we are in a danger zone where everyone lies to his neighbour. Great businesses do not just happen without trust; our greatest mistakes will happen because of quick trust. He said the same people who were praising Jesus were the ones who later crucified Him. Many times Jesus found Himself where people rejected Him because of His ideology.
He said we cannot succeed alone but we need good, inspired and informed people to succeed in life, which was why Jesus had 12 disciples. Those in whom we choose to trust should be led by God each day; when we trust them, we trust God.
TESTIMONIES

Healed Of Ovarian Cyst Through The Anointing Water
Mrs Ntisili Seng, a South African, was suffering from an ovarian cyst and had visited many gynaecologists for medical attention, who eventually recommended that she go for an operation. Her sister, in possession of the Anointing Water from The SCOAN rushed to her aid and  advised her to administer it in faith. To her surprise, the symptoms of the cyst disappeared and upon further medical examination, she was confirmed to be healed and without any trace of the ovarian cyst. Speaking to the congregation and viewers, she advised that people should not lose hope because God is always in control.

Healed Of Hypertension Through The Anointing Water
Mr Hassan Ola, from Warri, Delta State, had been suffering from hypertension for four years for which he could not get a solution. The heart disease had taken him to many places because it had deprived him of paying attention to his business, as he could not walk even for 30 minutes. He said he faced “troubles all over”.
He was lucky to obtain Anointing Water which God used to perform the divine miracle in his life. Today, he said, “I feel better. I can walk for more than one hour with no problem”. He said, “There is power in this water. You only need to believe.


Delivered From Fatal Accident Through The Anointing Water
Pastor Henry Neaba, based in Ebonyi State, Nigeria came to The SCOAN on January 2012 for “spiritual upliftment”. After receiving prayer from  Prophet T.B. Joshua, he returned home, believing that his case was settled. On March 12th, his boss had asked him to oversee a project at a site but felt strangely uneasy about the prospect. He decided to pray with Anointing Water in Jesus’ name to ward off the fear. He then boarded a okada (motorbike) to move to the site when, after five minutes, a car crashed into the bike. Pastor Henry flew off the motorbike, his head smashing into the windshield of the car. He went into a coma, his body slumped in a pool of blood. While in the coma, he saw himself on a spiritual journey which he could not understand but he kept shouting the name, Jesus. He saw a light and eventually saw T.B. Joshua who asked him to go back and pulled him to face where he was coming from.
Immediately he opened his eyes and slowly sat up to the amazement of the crowd of onlookers.  Unable to believe that he had survived such a traumatic accident, they rushed him to the hospital. When he was discharged, someone blessed him with a brand new car after hearing of surprising survival! He advised that people should believe in God as “any man who puts his trust in God will never be put in shame”.

Wednesday, June 27, 2012

MCHUNGAJI BURTON SANGA  NAPENDA KUWASHUKURU WOTE WALIHUSIKA KATIKA MSIBA WA MAMA YANGU MPENDWA AMBANGILE SANGA.

Shukrani zangu za dhati kwawale  wote waliokuwa pamoja nasi katika kumuuguza mama yangu alipokuwa hospitali ya Chimala Mbeya. Tunashukuru kwa kunifariji, kunichangia,kunitia moyo na maombi hasa pale mama alipokuwa amelazwa hospitalini.

Mbali na hapo ninawashukuru madaktari wote waliokuwa nami bega kwa bega kwa kumtibu mama yangu. Na pia namshukuru sana Dk. Mahenge kwa kujitoa nasi katika shughuli zote, tangia mama alipokuwa hospitalini mpaka anatoweka duniani. MUNGU AKUZIDISHIE PALE ULIPOTOA.

Napenda pia kutoa shukrani zangu za dhati kwa wote waliohudhuria katika mazishi ya mama yangu yaliyofanyika katika makaburi ya Itoroha Uyole Mbeya siku ya jumamosi 23 Juni 2012 pamoja na wachungaji wote, MUNGU WANGU NINAYEMTUMIKIA AWABARIKI.

Wenu katika Bwana
 MCH. BURTON SANGA


MSIBA ULIOMKUMBA BLOGGER WENU WA RUMAAFRICA, RULEA SANGA ALIPOFIWA NA MAMA YAKE MZAZI AMBANGILE LANZON SANGA
Hii ni siku ambayo siwezi kuisahau pale nilipompoteza mama yangu mzazi katika hospitali ya Chimala Mbeya siku ya ya Jumamosi 22 Juni 2012. Mama yangu alipata ugonjwa wa ghafla pale alipoaanza kutapika na baadae kukimbizwa dispensary na baada ya kupimwa aligundulika ana malaria mbili. Mama alirudishwa nyumbani na baada ya hapo usiku wake mama yangu hali iliaanza kubadilika na kuishiwa nguvu. Hali hiyo ilizidi kuwa mbaya na baadae kaka yangu Burton Sanga aliamua kukimbiza hospitali ya Chimala iliyoko Mbeya. Mama aliaendelea na matibabu na baadae kugundulika kuwa alikuwa na Blood Pressure (BP) na baada ya siku kama mbili aligundulika kuwa anaumwa Kisukari. Siku tatu baadae hali ya mama yangu ilikuwa mbaya sana.
Mama aliwekewa mpira ya Oxygen na mrija wa kupitisha chakula. Mama hakuweza kuongea kwa muda wote aliokuwa hospitali, lakini namshukuru sana Mungu wangu, baada ya kuniona mama alicheka kicheko cha maumivu na kuniambia "Mwanangu umekuja kuniuguza???" Nililia sana kumuona mama anavyoteseka na kuhema, kwani alikuwa anasumbuliwa sana na utoaji na uingizaji oxygen. Pia alikuwa analalamika na maumivu aliyokuwa anapata kutokana na kulalia mgongo kwa muda mrefu.
Siku ya Jumatano mama yangu hakuweza kuongea kitu chochote, macho yake yalikuwa yamefumba na mdomo wake ulikuwa umeachama kwaajili ya hewa. Mama alipochomwa na sindano na daktari kama nne begani hakuweza kushtuka wala kuhisi maumivu yote. Ndugu zangu walipokuwa wanatoa nguo zake mama alikuwa bado kafumba macho yake na hakuonyesha sign ya kuumia.
 
Nakumbuka kabla ya kifo cha mama yangu, ilikuwa ni siku ya Alhmaisi nilipomuombea sana mama yangu na kuwaaga baadhi ya ndugu zangu kuwa nataka niende Dar es Salaam kufuatilia pesa ambazo zitasaidia katika matibabu na siku ya jumatatu nitarudi tena Mbeya kuumuuguza mama yangu, lakini haikuwezekana. Ilipofika siku ya Ijumaa nilienda hospitalini kwaajili ya kumuaga mama yangu na ndugu zangu kuwa naenda Dar.
Nilipofika hospitalini nilikutana na shemeji yangu mke na kaka yangu Mchungaji Burton Sanga, alinikimbilia na kuniuliza "begi lako liko wapi?" na mimi nilimjibu "nimeliacha hotelini"  aliniangalia kwa huruma sana, na mimi nikaona baadhi ya ndugu zangu wako katika chumba cha kuhifadhia maiti. Shemeji aliniambia "Jipe moyo mama hayupo tena duniani" nililia sana kwa maana sikuamini kwani siku ya jana yake nilimuombea na kumshika mkono, kumbe ilikuwa ndio alama ya kuaagana 
Nilimshika mama yangu mkono kwa mara ya mwisho na usiku wa ijumaa mama aliaga dunia.
Siku ya Ijumaa ya 22 Juni 2012 mida ya saa 4:30am mama aliaga dunia, na sasa amepumzika katika makaburi yaliyoko Mbeya uyole kama unaelekea Tukuyu.
Mama ameacha watoto wanne, Yohana Sanga, Fidness Sanga, Burton Sanga na Rulea Sanga.
Blogger wenu nawaashukuru sana wale wote walionitumia pesa kwa kupitia Tigo Pesa kama rambirambi na maneno ya faraja ambayo yalinifariji sana. MUNGU WANGU ATAWALIPA
Ngoja tuone Safari nzima ilivyokuwa:

NIKIWA SAFARINI KUELEKEA MBEYA
 Nikiwa maeneo ya Morogoro
 Mishika ndicho kilikuwa chakula changu siku hiyo
Nikisubiri safari kuanza kuelekea Mbeya

MAMA AKIWA KATIKA HOSPITALI YA CHIMALA MBEYA
Mama yangu ambangile Lanzon Sanga akiwa amelazwa hospitalini Chimala Mbeya siku ya Jumamosi
 Kutoka kushoto ni wauguzi, dada yangu Aulelia Mahenge mtoto wa mama mkubwa, Binamu yangu, Mama Simda
 Shemeji yangu ambaye ni mke na kaka yangu Mchungaji Burton Sanga, Mama Judy.
Mama Judy amemlea mama yangu kwa muda wa miaka 17 tangia atoke Iringa na mpaka mauti imemchukua
Dada yangu Fidness Sanga akimwangalia mama 
 Blogger wenu Rulea Sanga (kulia) nikimtakia afya njema mama yangu

Daktari akimtibu mama yangu, pembeni ni shemeji yangu, mke na kaka yngu marehemu Amir Sanga a.k.a Short
 Daktari akiwa na baadhi ya ndugu na jamaa
PICHA BADO ZINAKUJA

Jifunze Kumiliki Majibu Ya Maombi Yako 2 -Mwl Sanga

Njia ya nne: Kumiliki muujiza kwa kuwatunza watumishi wa Mungu na kuchangia huduma mbalimbali.
Yoshua 12:1-3 kwenye ule mstari wa pili Biblia inasema “Basi wakamwandalia karamu huko naye Martha akamtumikia na Lazaro alikuwa mmoja wapo wa wale walioketi chakulani pamoja nao.
Hii pia ni habari nyingine inamhusu Lazaro ambaye Yesu alikuwa amemfufua baada ya kuwa amekufa kwa siku nne. Sasa Lazaro aliumiliki muujiza wake wa kufufuliwa kwa kumtunza Yesu pamoja na wanafunzi wake kumi na wawili. Hii ina maana Lazaro pamoja  na dada zake waliingia gharama kwa ajili ya kuwatunza Yesu pamoja na  wanafunzi wake, Kwa siku zote ambazo Yesu alikaa kwa Lazaro, Lazaro alihakikisha hawalali njaa, anawapa mahali pa kulala nk.


Sasa unaweza kumiliki muujiza wako kwa kuruhusu watumishi wa Mungu wakae nyumbani kwako. Huenda wamekuja kwenye mkutano au semina kwa wiki moja au mbili itoe nyumba yako itumike, kufanya hivyo ni kumfanya Mungu aendelee kukulinda wewe na yale aliyokupa maana anajua hutamnyima siku moja atakapohitaji kuvitumia. Wapo wengine wanaomiliki kwa kutoa magari yatumike kipindi chote cha mikutano, unaweza pia  kumiliki kwa kuchangia gharama za mikutano  si lazima pesa lakini hata kufanya kazi mbalimbali katika mkutano huo, huenda  ni  usafi,  kubeba vyombo, kufanya usafi walikofika watumishi, kuombea huo mkutano au semina nk. Nakuambia unaweza ukaona kama ni vitu vidogo lakini ndivyo mujibu ya maombi yanavyomilikiwa bila kujali Mungu amekutendea nini.

Nija ya tano: Kumiliki muujiza kwa kufanya  maamuzi ya kuokoka endapo Mungu alikufanyia huo muujiza kabla hujaokoka, na kuwaambia wengine habari ya Yesu aliyekuponya.

Ukisoma ile sura nzima ya 9 ya kitabu cha Yohana utakutana na habari ya kipofu mmoja tangu kuzaliwa kwake  ambaye Yesu alikuwa amemponya. Ule mstari wa 39 unasema “akasema,Naamini, Bwana akamsujudia” Ukisoma vizuri habari hii utagundua baada ya mahojiano marefu kati ya mafarisayo na yule kijana kuhusu uponyaji wake ndipo Yesu akamwuuliza je unamwamini mwana wa Mungu? Yule kijana akamwuliza ni nani huyo nipate kumwamini? Kwa kifupi Yesu akamjibu unayezungumza naye. Ndipo yule kijana  akasema, naamini Bwana akamsujudia.

Mtu mwingine ni Naamani ambaye tumekwisha ona habari zake, kitendo cha yeye kusema toka leo sitatoa sadaka kwa miungu  ya shamu ila kwa Bwana  ni dalili  ya kuonyesha kumwamini Mungu wa Israel. Hivyo hata leo wapo ambao Mungu anawatendea mambo mengi hata kabla hawajaokoka sasa ili kumiliki  hayo ambayo Mungu amekufanyia mwamini Yesu ndio huo muujiza utadumu. Wapo watu leo wanafunguliwa kwenye nguvu za mapepo huo ni  uponyaji. Sasa badala ya kuwasaidia watu wamwamini Yesu tunawaacha, nakuambia pepo watarudi kwa huyo mtu wenye nguvu zaidi kuliko yule wa kwanza.


Pia ukisoma vizuri habari hiyo hiyo utagundua kwamba huyu jamaa alimiliki uponyaji wake kwa kuwaambia wengine habari za Yesu na kukiri kwamba  mponyaji ni Yesu na si mtu mwingine, nakuambia  kufanya  hivyo ni kujihakikishia kudumu kwa huo muujiza na Mungu ataendelea kuutunza huo muujiza  maana wewe ni chombo chake. Mungu akikuponya au kukubariki usinyamaze kimya waambie wengine habari za Yesu aliyekuponya. Jifunze kutoka kwa mwanamke msamaria. Uponyaji wa nafsi yake ulipelekea watu wengi wa mji wa Samaria kuokoka. Soma kile kitabu cha Yohana sura ya nne mistari 30 ya kwanza utaiona habari hii.

Mpenzi msomaji wangu mpaka hapa naamini utakuwa umepata kitu cha kukusaidia labda nikuambie hivi  siri kubwa ya mafanikio ni kuliweka neno la Mungu kwenye matendo, si unajua imani pasipo matendo imekwisha kufa katika nafsi ya huyo mtu mwenye imani hiyo. Nimeamua  kuandika ujumbe  huu baada ya kuona wana wa Mungu wengi imefika mahali  wanakuta yale ambayo Mungu aliwapa kama majibu ya maombi yao yameshaharibiwa na shetani, wapo waliozaa watoto wao wakafa na walimuomba sana Mungu kuhusu hao watoto nk. Sasa  ni imani  yangu kwamba tangu sasa jambo lolote ambalo Mungu atakupa kama jibu la maombi yako utalimiliki.
Ndimi katika huduma

Mwl Patric Sanga

MCHUNGAJI BURTON SANGA ANAWAKARIBISHA KATIKA BLOG YAKE MPYA
www.vanyasanga.blogspot.com

Nawasalimu kwa Jina laYesu Kristo. Mimi ni Mchungaji wa kanisa la TAG lililoko Mbeya Uyole eneo la Gombe.

Blog yangu itajihusisha na mambo yafuatayo
1 Mahubiri
2. Shuhuda mbalimbali
3. Matamasha mbalimbali
4. Mikutano ya Injili
5. Habari mbalimbali za Mungu
6. Vipindi nivyohubiri kwa kupitia radio mbalimbali
7. Huduma za Kiroho.n.k


Unaweza kuwasilina nami kwa:-
Barua Pepe: burtonsanga.gmail.com
Simu: +255 755 874809

VANYASANGA POST TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...