Tuesday, August 21, 2012

MTANZANIA ATOA USHUHUDA WAKE WA KUTOTOKWA NA DAMU BAADA YA KUANGALIA EMMANUEL TV YA TB JOSHUA

Mtafsiri: Blogger Rulea Sanga

Hapa kuna ushuhuda wa ajabu wa mtazamaji wa Emmanuel TV kutoka Tanzania ambaye alipokea ukombozi na uponyaji kwa kuangalia Emmanuel TV.

"Jina la Yesu lisifiwe! Ningependa kutoa shukrani zangu kwa timu nzima ya Emmanuel TV, Nabii T.B. Joshua na Wise Men kwa kazi ya Mungu na utayari wa kusaidia wengine"

Ninaushuhuda mkubwa sana ambao ningependa kushirikiana kwa ukombozi nilioupata kwa kuangalia Emmanuel TV! Ilikuwa siku ya Jumatatu 13/08/2012 wakati wa  "Live Service" , nilipokuwa naangalia Emmanuel TV wakati "Wise Men" walipokuwa wanawahudumia watu waliokusanyika pale. Nilimwona dada kutoka Zambabwe ambaye alikuwa na tatizo kama langu ambalo ni kutokwa na damu kutokana na roho ya mwanaume. Nilikuwa nikimuota huyu mwanaume katika ndoto zangu kwa miaka mingi sasa na nilikuwa nikitokwa na damu mfululizo kwa muda mrefu. Nilikuwa naogopa kwenda kulala kwasababu nilikuwa najua utakuwa usiku wa mateso na shida.

"Kwahiyo  "Wise Man" John Chi alipokuwa akimwombea yule mwanamke, imani yangu ikaanza kukua. Nilikuwa nalichukia hili pepo ambalo lilikuwa likinitesa mimi! Nilijisemesha mwenyewe, 'Kama huyu mwanamke atakombolewa, na mimi nitakuwa nimekombolewa.' Na alipokuwa anaombewa, nilianguka chini katika chumba changu! Siwezi kuelezea kitu gani kilinitokea lakini nguvu za Mungu zilinipiga katika mwili wangu. Na mwanamke wa Zimbabwe aliposema yuko huru kwa jina la Mungu, na mimi nikaanza kumshukuru Mungu kwa kukombolewa kwangu. Na mara alipokuwa amewekwa huru, na mimi nikawekwa huru!
"Kwa utukufu wa Mungu mpaka sasa, sitokwi tena na damu, na sioti tena ndoto mbaya tena. Nina furaha ya kutosha na amani katika moyo wangu. Jina la Yesu na liinuliwe na kutukuzwa milele na milele!" Aminia

Peace Gresmo, Tanzania
---------------------------------------------------------------------------

Spiritual Husband Exposed; Excessive Bleeding Stopped!

Here is a wonderful testimony from an Emmanuel TV viewer in Tanzania who received her deliverance and healing through watching Emmanuel TV:
“Praise the name of the living Jesus! I would like to extend my special thanks to the Emmanuel TV team, Prophet T.B. Joshua and also all the Wise Men for their commitment to God and readiness to serve others.
“I have a wonderful testimony to share about the deliverance I received through watching Emmanuel TV! Well, it was on Monday 13th August during the live service when I was watching Emmanuel TV as the wise men were ministering to the congregation. I saw a lady from Zimbabwe who had been tormented by exactly the same case as I had, which was a spiritual husband that caused excessive bleeding. I had been tormented by this strange man in my dreams for many years and had been bleeding continually for so long. I was always afraid of going to sleep because I know it would be a night of torment.
“So, when Wise Man John Chi was praying for her, faith began to rise in my heart. I was angry at this demon that was tormenting me! I said to myself, ‘If this lady will be delivered, I also will be delivered.’ As she was being prayed for, I suddenly fell down in my room! I can’t explain what happened but the power of God hit my body. As the lady from Zimbabwe was declared free by the man of God, I also started thanking God for my deliverance. As soon she was set free, I also was set free!
“To the glory of God, up to this moment, I am no longer bleeding and am not experiencing any bad dreams or nightmares anymore. There is so much joy and peace in my heart. May the name of Jesus be lifted on high and glorified forever and ever, amen!”
Peace Gresmo, Tanzania

No comments:

Post a Comment

VANYASANGA POST TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...