Sunday, August 26, 2012

MUIGIZAJI WA NIGERIA, TONTO DIKEH AFUNGULIWA KUPITIA EMMANUEL TV

Mtafsiri: Rulea Sanga

Muigizaji wa Nollywood, Toto Diken alisema katika mahojiana kutoka na kuokolewa kwa kuacha kuvuta sigara baada ya kuomba pamoja na TB Joshua kwa kupitia Emmanuel TV. Kutokana na Tonto ambaye alianza kuvuta sigara akiwa na umri wa miaka 13, alijiunga na Nabii TB Joshua katika maombi kwa kupitia Emmanuel TV na alipokea muujiza wake katika hali ambayo hakutegemea.

Aliliambia gazeti la Burudani la Nigeria, "Nilikuwa sivuti sigara mwenyewe, Nilikuwa naangalia kipindi katika TV cha Nabii TB Joshua na alikuwa amenyoosha mikono kwa watu huku akiwaobea. Huwa napenda kuangalia vipindi vyake katika Emmanuel TV. Alipokuwa akiomba, alisema, 'Nyoosha mikono yako katika T' nikanyoosha mikono yangu siku hiyo. Hasa nilikuwa nahitaji kitu kingine kutoka kwa Mungu, na sio kuvuta sigara kwasababu napenda kuvuta! Baada ya maombi nilikaa nilipokuwa nimekaa na nikajisikia kulala usingizi. "Baada ya maombi Tonto aliamka na akajisikia kuvuta kama kawaida yake, kitu cha kujua au kugundua ni kwamba hiyo ilikuwa ni tabia yake kwa muda wa miaka 14 ya kuvuta." Nilipoamka, nilichukua sigara na nikajisikia kama nimechanganyikiwa. Sikujigundua hata kuwa nimechukua hiyo sigara kwaajili ya kuvuta. Niliona kama sumu"


One of Nollywood’s rising actresses, Tonto Dikeh, revealed in an interview that she was delivered from an addiction to smoking through praying along with Prophet T.B. Joshua on Emmanuel TV. Glory be to God!According to Tonto, who started smoking at the tender age of 13, she joined Prophet T.B. Joshua to pray on Emmanuel TV and received the miracle in a way she never expected.
She told a Nigerian entertainment magazine, “I didn’t quit smoking by myself. I was watching a program on TV with Prophet T.B. Joshua and he was laying hands on people and praying for them. I love to watch his programs on Emmanuel TV. When he was praying, he said, ‘Lay your hands on the TV’ and I just laid my hands that day. I actually needed something else from God, not to quit smoking because I loved smoking! However, after praying I sat back and I think I slept off.”After the prayer, Tonto woke up and attempted to smoke as usual, only to discover that the very habit that had been part of her for 14 years suddenly became revolting. “When I woke up, I took a stick of cigarette and I felt crazy. I couldn’t even imagine that I took it up to smoke in the first place. It felt like poison!”

WAINJILISTI KUTOKA SCOAN KWA NABII T.B. JOSHUA KUINGIA TANZANIA

Mwandishi: Rulea Sanga

Watanzani tunaugeni mkubwa sana kutoka kwa Nabii TB Joshua. Hawa si wengine ni WAINJILISTI ambao wanakuja kutuhudumia Watanzania. Hii ni baraka tumepewa na Mungu kwa watu kama hawa kuingia nchini kwetu.

Tumekuwa tukiwaangalia katika Emmanuel TV kwa muda mrefu na tumekuwa tukitamani kuwaona uso kwa uso. Nisikuchoshe kwa maneno mengi mdau wangu, ngoja nikupe mchakato mzima 
Unatakiwa kufika Jumatatu 27.08.2012 saa moja katika ofisi za TB Joshua Dar es Salaam, na wale waliojiandikisha kwenda SCOAN Nigeria  waje pia na medical report zao eneo la Water Front jijini Dar es Salaam.
Wainjilisti watakutana na wale  waliojiandikisha kwenda SCOAN Nigeria siku ya Jumanne Diamond Jubilee.
Watanzania naomba tufike ili kupata ujumbe kutoka kwa watumishi wa Mungu. Mungu wangu awabariki.

Mimi kama blogger nawatia moyo kufika, kumbukeni na mimi nilipata muujiza wa kuonana na Nabii TB Joshua mwezi Aprili 2012


SCOAN-Nigeria

BBlogger Rulea Sanga nilipokuwa SCOAN Nigeriahttps://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh3g_1qEmAEtpb9iZ8V8tibGLVX9JLu3LGfaSB9NXxf6JvmJhVIeRrbEFmuLPqhA08D6YvqBGRnPiCXrYIUqq4w7GBWmW1XyTIgKNgqlYi3uCidF-CrGVfii9TGS9QMGDpMF1sQugrEuZ6T/s1600/five_wise_men_SCOAN.jpg
Wise Men

Ndani ya Sinagogi

Kwaya ya SCOAN

Watu wengi wamepona kwa kupitia Emmanuel TV hasa pale unapogusa mkono wa Nabii TB Joshua ambao huunyosha katika screen yako

Tuesday, August 21, 2012

MTANZANIA ATOA USHUHUDA WAKE WA KUTOTOKWA NA DAMU BAADA YA KUANGALIA EMMANUEL TV YA TB JOSHUA

Mtafsiri: Blogger Rulea Sanga

Hapa kuna ushuhuda wa ajabu wa mtazamaji wa Emmanuel TV kutoka Tanzania ambaye alipokea ukombozi na uponyaji kwa kuangalia Emmanuel TV.

"Jina la Yesu lisifiwe! Ningependa kutoa shukrani zangu kwa timu nzima ya Emmanuel TV, Nabii T.B. Joshua na Wise Men kwa kazi ya Mungu na utayari wa kusaidia wengine"

Ninaushuhuda mkubwa sana ambao ningependa kushirikiana kwa ukombozi nilioupata kwa kuangalia Emmanuel TV! Ilikuwa siku ya Jumatatu 13/08/2012 wakati wa  "Live Service" , nilipokuwa naangalia Emmanuel TV wakati "Wise Men" walipokuwa wanawahudumia watu waliokusanyika pale. Nilimwona dada kutoka Zambabwe ambaye alikuwa na tatizo kama langu ambalo ni kutokwa na damu kutokana na roho ya mwanaume. Nilikuwa nikimuota huyu mwanaume katika ndoto zangu kwa miaka mingi sasa na nilikuwa nikitokwa na damu mfululizo kwa muda mrefu. Nilikuwa naogopa kwenda kulala kwasababu nilikuwa najua utakuwa usiku wa mateso na shida.

"Kwahiyo  "Wise Man" John Chi alipokuwa akimwombea yule mwanamke, imani yangu ikaanza kukua. Nilikuwa nalichukia hili pepo ambalo lilikuwa likinitesa mimi! Nilijisemesha mwenyewe, 'Kama huyu mwanamke atakombolewa, na mimi nitakuwa nimekombolewa.' Na alipokuwa anaombewa, nilianguka chini katika chumba changu! Siwezi kuelezea kitu gani kilinitokea lakini nguvu za Mungu zilinipiga katika mwili wangu. Na mwanamke wa Zimbabwe aliposema yuko huru kwa jina la Mungu, na mimi nikaanza kumshukuru Mungu kwa kukombolewa kwangu. Na mara alipokuwa amewekwa huru, na mimi nikawekwa huru!
"Kwa utukufu wa Mungu mpaka sasa, sitokwi tena na damu, na sioti tena ndoto mbaya tena. Nina furaha ya kutosha na amani katika moyo wangu. Jina la Yesu na liinuliwe na kutukuzwa milele na milele!" Aminia

Peace Gresmo, Tanzania
---------------------------------------------------------------------------

Spiritual Husband Exposed; Excessive Bleeding Stopped!

Here is a wonderful testimony from an Emmanuel TV viewer in Tanzania who received her deliverance and healing through watching Emmanuel TV:
“Praise the name of the living Jesus! I would like to extend my special thanks to the Emmanuel TV team, Prophet T.B. Joshua and also all the Wise Men for their commitment to God and readiness to serve others.
“I have a wonderful testimony to share about the deliverance I received through watching Emmanuel TV! Well, it was on Monday 13th August during the live service when I was watching Emmanuel TV as the wise men were ministering to the congregation. I saw a lady from Zimbabwe who had been tormented by exactly the same case as I had, which was a spiritual husband that caused excessive bleeding. I had been tormented by this strange man in my dreams for many years and had been bleeding continually for so long. I was always afraid of going to sleep because I know it would be a night of torment.
“So, when Wise Man John Chi was praying for her, faith began to rise in my heart. I was angry at this demon that was tormenting me! I said to myself, ‘If this lady will be delivered, I also will be delivered.’ As she was being prayed for, I suddenly fell down in my room! I can’t explain what happened but the power of God hit my body. As the lady from Zimbabwe was declared free by the man of God, I also started thanking God for my deliverance. As soon she was set free, I also was set free!
“To the glory of God, up to this moment, I am no longer bleeding and am not experiencing any bad dreams or nightmares anymore. There is so much joy and peace in my heart. May the name of Jesus be lifted on high and glorified forever and ever, amen!”
Peace Gresmo, Tanzania

Thursday, August 2, 2012

MAANA YA NAMBA 666


comments
Maandiko yanasema: ... siku za mwisho watakuja na dhihaka zao watu wenye kudhihaki, wafuatao tamaa zao wenyewe na kusema, Iko wapi ahadi ile ya kuja kwake? Kwa maana, tangu hapo baba zetu walipolala, vitu vyote vinakaa hali iyo hiyo, tangu mwanzo wa kuumbwa. (2 Petro 3:3-4).

Mtume Petro anatuambia hapa kwamba, watu watasema, “Kila siku mnasema, Yesu anakuja; Yesu anakuja. Yuko wapi? Mbona miaka inaenda tu. Msituzingue bwana!”
Je, hayo si ndiyo tunayoyasikia kila uchao? Mimi nimeshayasikia mara kadhaa. Naamini nawe pia umesikia dhihaka kama hizo.

Lakini maandiko yanasema kwamba: Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake, kama wengine wanavyokudhani kukawia, bali huvumilia kwenu, maana hapendi mtu yeyote apotee, bali wote waifikilie toba. (2 Petro 3:9).

Mungu anataka watu wote wamwamini Yesu na kupokea wokovu wa bure ambao Yeye aliulipia gharama kubwa ya uhai wake. Lakini nikwambie jambo: siku atakapotokea, hata kama kwa mtazamo wa kibinadamu ataonekana anachelewa, muda wote wa nyuma hautamfaidia kitu kamwe mtu ambaye hakumwamini Yeye ajaye! Cha msingi ni je, wakati huo atakukuta katika mkao gani kiimani?utakavyokuwa wakati huo ndicho kitakachoamua hatima yako ya milele!

Katika nyakati hizi tulizo nazo, dunia inajiandaa kuingia wakati wowote kwenye kipindi ufalme wa kuzimu wa moja kwa moja. Shetani atakuwa anatawala dunia moja kwa moja.

Kwa sasa, japo shetani yupo na anatenda kazi, lakini ni kwa kiwango cha chini. Maandiko yanasema: Maana ile siri ya kuasi hivi sasa inatenda kazi; lakini yuko azuiaye sasa, hata atakapoondolewa. Hapo ndipo atakapofunuliwa yule asi, ambaye Bwana Yesu atamwua kwa pumzi ya kinywa chake, na kumwangamiza kwa ufunuo wa kuwapo kwake; yule ambaye kuja kwake ni kwa mfano wa kutenda kwake Shetani, kwa uwezo wote, na ishara na ajabu za uongo; na katika madanganyo yote ya udhalimu kwa hao wanaopotea; kwa sababu hawakukubali kuipenda ile kweli, wapate kuokolewa. (2 Wathesalonike 2:6-12).

Sasa huyu asi anapitia wapi? Biblia inasema kwamba: Maana shina moja la mabaya ya kila namna ni kupenda fedha; ambayo wengine hali wakiitamani hiyo wamefarakana na Imani, na kujichoma kwa maumivu mengi. (1 Timotheo 6:10).
Fedha ni kitu kizuri na muhimu sana katika maisha yetu. 

Lakini hapo pia ndipo penye nguvu na mlango wa kuzimu. Fedha au biashara au kwa túseme uchumi, vitahusika sana katika nyakati za mwisho za utawala wa shetani hapa duniani. Huu ni utawala ambao kimsingi maandalizi yake ni kama yameshakamilika.

Bwana Yesu ameshatupa taarifa juu ya kile kinachoitwa “chapa ya mnyama” ambayo watu watatakiwa kuwa nayo.
Imeandikwa: Naye awafanya wote, wadogo kwa wakubwa, na matajiri kwa maskini, na walio huru kwa watumwa, watiwe chapa katika mkono wao wa kuume, au katika vipaji vya nyuso zao; tena kwamba mtu awaye yote asiweze kununua wala kuuza, isipokuwa ana chapa ile, yaani jina la mnyama yule, au hesabu ya jina lake. Hapa ndipo penye hekima. Yeyé aliye na akili, na aihesabu hesabu ya mnyama huyo; maana ni hesabu ya kibinadamu. Na hesabu yake ni mia sita, sitini na sita. (Ufunuo 13:16-18).

Utendaji wa huyu asi umejikita kwenye kudhibiti fedha; uchumi wa dunia.

Namba 666 hadi sasa iko sehemu mbalimbali – hususani kwenye sekta ileile ya pesapesa, yaani biashara na uchumi.
Kama ninavyosema kwenye makala yangu mbalimbali, lengo kuu la shetani ni kuwasomba wanadamu wengi kadiri iwezekanavyo na kuwaingiza kuzimu, na hatimaye jehanamu ya motoni ambako yeye alishahukumiwa kuwa ndiko mahali pake pa milele.

Lakini ili aweze kuwapata wengi, lengo la kwanza lilikuwa ni kuwadanganya wanadamu ili wasimwamini Mungu – kazi ambayo ameshaifanya kwa mafanikio makubwa tu. Hata hivyo, kwa vile shauku yake bado ni kubwa mno, lengo lake la pili ni kuutawala ulimwengu kwa ukaribu na uwazi zaidi kuliko alivyofanya hadi sasa. Ndio maana hivi sasa kuna ajenda ya “new world order” ambayo iko mbioni kutekelezwa.
 Mpango huu una malengo kadhaa, yakiwamo yafuatayo:
  • Kuwa na serikali moja inayotawala dunia nzima; ambayo katika ndoto ya Nebukadreza iliyofasiriwa na Danieli, ni ule ufalme wa mwisho wa vidole vya chuma kilichochanganyika na udongo(Dan. 2:33).
  • Kuwa na uchumi mmoja duniani kote.
  • Kuwa na jeshi moja la dunia nzima.
  • Kuwa na dini moja duniani kote (huenda umeshasikia juhudi mbalimbali ambazo zinafanywa sasa za kuanzisha dini hiyo, jambo ambalo linaungwa mkono na Umoja wa Mataifa). Hii ndiyo ambayo Bwana katika Ufunuo anaiita kahaba mkuu. (Ufu. 17:5).
Haya yote ni sehemu ya kutekeleza mpango wa kumleta kiongozi wa kishetani, yaani mpinga Kristo (yule asi), ambaye ataongoza dunia nzima.
Ili kuweza kudhibiti uchumi wa dunia yote pamoja na wanadamu watakaokuwapo wakati huo, inabidi uwepo mfumo wa kumfuatilia kila atakayekuwapo.

Kwa kuwa Bwana Yesu ameshatuambia kuwa hesabu ya jina la mnyama huyo ni 666, swali ni kuwa, je, kuna kitu kama hicho hivi sasa? Jibu ni ndio. Na ni mfumo ambao tunaukuta kulekule kwenye sekta ya biashara.

Mfumo huu umekuwapo duniani kwa muda mrefu sasa, huku ukiendelea kuboreshwa zaidi na zaidi kama ilivyo kwa teknolojia nyingine.

Chukua bidhaa mbalimbali – iwe ni gazeti, dawa ya meno, maji ya kunywa, mafuta ya kujipaka, sabuni ya kuogea, n.k., ukiangalia kwenye makasha au kwenye bidhaa zenyewe, utaona kitu kama hiki:
 
Hii ni kodi ya mistari (bar code). Kodi hii ina sehemu kuu mbili – sehemu ya kushoto na sehemu ya kulia. Sehemu hizo zimezungukwa na mistari mirefu zaidi ya mingine.

Namba unazoziona chini ya mchoro, upande wa kushoto, ni thamani ya mistari iliyo juu yake. Kila namba inawakilishwa na mistari miwili ya unene fulani na iliyotenganishwa na nafasi ya kiasi fulani. Mambo hayo matatu, yaani: mistari kuwa miwili, unene wa mistari na nafasi kati yake, hayabadiliki (suala la urefu halihusiki). Kwa hiyo, popote utakapoikuta mbili, mistari yake itakuwa na unene uleule na nafasi ileile kwa upande wa kushoto.
Hali kadhalika, kwa upande kulia nako namba zinakuwa na tabia hizo tatu lakini hazifanani na zile za kushoto. Tabia za kushoto ni za kushoto, na za kulia ni za kulia.
Lakini ningependa uangalie ile mistari mirefu mitatu. Ukiichunguza utaona kuwa inafanana kwa unene na nafasi kati yake. Hii inamaanisha kuwa inawakilisha namba ileile.

Sasa ili kujua hiyo ni namba gani, angalia kwenye kodi za bidhaa mbalimbali upande wa kulia (sio wa kushoto). Kisha angalia sehemu zote zenye 6. Chunguza mistari inayowakilishwa na 6. Utaona kuwa inafanana kabisa na ile iliyo mirefu. Hiyo itakuonyesha kuwa kumbe ile mistari mirefu ya katikati ni 666.

Kama nilivyodokeza hapo juu, hii ni sehemu mojawapo tu ambapo 666 inatumika.

Lakini tunachoweza kuona ni kwamba huu si mwonekano wa mwisho (final form) ya kile kitakachotumiwa na mpinga Kristo wakati wa kuitawala dunia.  

Chapa halisi ya mpinga Kristo, inadhaniwa na wengi kuwa itakuwa ni ‘electronic chip’ ndogo ambayo, kama anavyosema Bwana Yesu mwenyewe, itaweza kuwekwa kwenye mkono au usoni (hii inaonyesha kuwa ni kitu kitakachopandikizwa chini ya ngozi). Lakini bila shaka, kifaa hicho nacho kitakuwa na tabia zilezile za barcode; japo inaweza isifanane moja kwa moja na barcode za sasa.

Tabia mojawapo muhimu ya barcode ni kuwa inasomeka kielektroniki. Unapoenda kwenye supermarket, mhudumu huelekeza kwenye barcode kifaa kinachotoa namna ya mionzi fulani. Kwa sekunde moja kinasoma kila taarifa kuhusiana na bidhaa uliyochagua, kwa mfano bei yake, nk.

Lakini kwa sababu teknolojia ya chapa ya mnyama itakuwa ya juu zaidi, wale wadhibiti wa ulimwengu katika kipindi hicho, wataweza kufuatilia nyendo za kila mtu atakayekuwa amewekewa hicho kifaa.

Nihitimishe sehemu hii kwa kusema kwamba, barcodes zilizomo kwenye bidhaa madukani sasa hivi sio chapa halisi ya mpinga Kristo bali ilikuwa ni sehemu ya maandalizi ya teknolojia itakayotumika (ambayo tayari ipo kazini).

Lakini kama nilivyokueleza kwenye makala yangu ya mwisho kuhusu alama za kishetani (kama hukusoma unaweza kusoma hapa), shetani amekuwa kwenye harakati zake za kumharibu mwanadamu kwa miaka na miaka. Hizi barcodes zimekuwapo kwa muda mrefu, lakini  ni sehemu kabisa ya mpango wake huo wa uharibifu – japo wengi wanaweza kuzitazama kama maendeleo ya kawaida ya kiteknolojia yaliyoletwa na mwanadamu. Kumbuka siku zote, shetani ni kerubi afunikaye. (Ezekieli 28:14).

Katika sehemu ya pili na ya mwisho ya makala haya, nitakueleza jinsi ambavyo hivi sasa teknolojia imefikia juu zaidi na tayari watu wanaanza kupandikiziwa hizo ‘chip’. Usikose sehemu hiyo.

Rafiki, usilale. Shetani anakuja; na Yesu naye anakuja! Kama wewe ni mmoja wa wale wanaosema kuwa Biblia ni uongo; au kwamba Biblia imechakachuliwa, hakuna tena muda wamalumbano na mabishano. Fungua macho yako utazame upya sawasawa! Kila kitu kiko wazi sasa!

Yafuatayo ni maneno ya Bwana wa Mbingu na nchi: Kwa maana, amin, nawaambia, Mpaka  mbingu na nchi zitakapoondoka, yodi moja wala nukta moja ya torati haitaondoka hata yote yatimie. (Mathayo 5:18).
Kila alichokisema Mungu wa mbinguni kwenye Biblia NI LAZIMA kitimie! Na mengine ndiyo haya tunashuhudia mbele za macho yetu.

 Endelea kufuatilia pia masomo ninayoweka kwenye blog ya: www.injiliyakweli.blogspot.com na pia www.truthofgospel.blogspot.com. Ukiwa na maoni au chochote, unaweza pia kuniandikia kupitia

Tuesday, July 31, 2012

CHEMSHA BONGO NA BIBLE

Mtunzi wa Mtihani: Rulea Sanga

MITIHANI WA MWISHO WA MWEZI JULAI 2012 WA CHEMSHA BONGO NA BIBLE
Unatakiwa kujibu maswali yote kwa muda wa saa mbili na nusu. Tunaamini utazingatia hilo agizo kwasababu wewe ni mtumishi wa Mungu.

Majibu yako unaweza kunitumia katika email yangu rumatz2011@yahoo.com.

Angalia muda ulioanza kujibu kwa makini.

Kumbuka hapo ulipo unasimamiwa na Roho Mtakatifu kwahiyo huwezi kufanya jambo lakuangalizia.


Ukiangalizia Roho Mtakatifu na nguvu za Mungu zitakutoa katika chumba chako cha kufanyia mtihani.

Matokeo yako utatumiawa kwa email na utapewa na cheti cha kufanya mtihani.

Kila swali lina maksi 10

Jinsi ya kujibu: Unatakiwa kuchagua jibu sahihi na ukipata andika namba ya jibu na jibu lake kwa kuandika herufi kama ni A, B, au C. Na usiandike swali, wewe tutumie hiyo herufu na namba ya swali.


MASWALI YOTE NI YA KUCHAGUA

Chagua jibu sahihi;

  1. Kitu gani kilitokea wakati Yesu anabatizwa

                 (a) Wingu jeusi

                  (b) Tetemeko la ardhi

                  (c) Mbingu za dunia zikamfunukia akaona Roho wa Mungu akishuka             
                 kama hua, akija juu yake, na sauti kutoka juu ikisema, Huyu ni
                 mwanagu mpendwa wangu, ninayependezwa naye

  2. Yesu alipopandishwa na Roho nyikani ili ajaribiwe na ibilisi, alifunga kula siku ngapi?

                  (a) kumi

                  (b) Sita

                  (c) Arobaini
  3.   (i) Yesu alipoingia Kapernaumu, akida mmoja alimjia, akimsihi akisema, Bwana mtumishi wangu amelala, mgonjwa wa kupooza, anaumwa sana. Yesu akamwambia,

                  (a) Amini ameshapona

                  (b) Nitakuja, nimponye

                  (c) Nitakuja, nimuokoe na atapona.

    (ii) Yule akijibu akasema, Bwana mimi sistahili wewe uingie chini ya dari yangu, lakini sema neno na mtumishi wangu atapona. Yesu aliposikia hayo alistajabu akawambia wale waliomfuata

                  (a) Amini na wambie sijaona imani kubwa kama hii kwa yeyote
                 katika Israel

                  (b) Amini na wambie sijaona imani kubwa kama hii kwa yeyote
                 katika mkutano huu

                  (c) Amini na wambie sijaona upendo kubwa kama huu kwa yeyote
                 katika Israel

  4. (i) Kuna muujiza ambao Yesu aliufanya wa kuiongeza mikate na samaki ambapo wanafunzi wake walikula mpaka wakasaza. Ni mikate mingapi na samaki ngapi ambazo Yesu aliziombea kwa kutazama juu mbinguni kwa Mungu?

                  (a) Mikate miwili na samaki watano

                  (b) Samaki wawili na mikate mitano

                  (c) Mkate mmoja na samaki waili

    (ii) Masazo yaliyobaki baada ya wanafunzi kula na kushiba ilijaa vikapu vingapi?

                  (a) kumi na viwili

                  (b) Kuma na saba

                  (d) viwili

  5. Ni baada ya kufanya nini, Yesu aliwaambia, “Imeandikwa, nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala, bali ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang’anyi”.

                  (a) Ni baada ya Yesu kuingia hekaluni na kuona watu wakiuza na
                 kununua, Yesu akapindua meza za wabadili fedha na viti vyao
                 waliokuwa wanauzia njiwa

                  (b) Ni baada ya Yesu kuingia msikitini na kuona watu wakiuza na
                 kununua, Yesu akapindua meza za wabadili fedha na viti vyao
                 waliokuwa wanauzia njiwa

                  (c) Ni kabla ya Yesu kuingia hekaluni na kuona watu wakiuza na
                 kununua, Yesu akapindua meza za wabadili fedha na viti vyao
                 waliokuwa wanauzia njiwa
  6. (i) Yuda alipoona ya kuwa Ysu amekwisha kuhukumiwa, alifanya nini?

                  (a) Yuda alijuta akawarudishia wakuu na makuhani na wazee vile
                 vipande thelathini na moja vya fedha

                  (b) Yuda alijuta akawarudishia wakuu na makuhani na wazee vile
                 vipande thelathini vya fedha

                  (c) Yuda alijuta akawarudishia wakuu na makuhani na wazee vile
                 vipande thelathini vya dhahabu

    (ii) Ni maneno gani Yuda alisema baada ya kurudisha vile vipande alivyopewa kwaajili ya kumsaliti Yesu?

                  (a) Alisema, Nalikosa nilipoisaliti damu isiyo na hatia
                  (b) Alisema, Sijakosea nilipoisaliti damu isiyo na hatia
                  (c) Alisema, Nalikosa nilipoisaliti damu iliyo na hatia

    (ii) Yuda baada ya kukimbia ndani ya hekalu kutokana na kumsaliti Yesu alifanya nini?

                  (a) Alikimbia na kujinyonga

                  (b) Alirudi na kumsujudia Yesu

                  (c) Alihuzunika sana na kulia

  7. Baada ya kusikia kuwa Herode amekufa Misri, Yusufu, Yesu na Bikira Maria  walitoka Israel ni wapi walienda kuishi?

                  (a) Nazareti

                  (b) Misri

                  (c) Marekani
  8. Taja majaribu matatu ambayo Yesu alijaribiwa na Ibilisi nyikani?

                  (a) (i) Mawe yawe mikate

                      (ii) Yesu kujitupa chini kutoka katika kinara cha hekalu

                      (iii) Kumsujudia Ibilisi

                  (b) (i) Mchanga uwe mikate

                      (ii) Yesu kujitupa chini kutoka katika kinara cha mlima

                      (iii) Kumsujudia Ibilisi

                  (c) (i) Mawe yawe mikate

                      (ii) Yesu kujitupa chini kutoka katika kinara cha hekalu

                      (iii) Kumsujudia Mfalme
  9. Yesu aliposhuka mlimani, makutano mengi walimfuata. Na tazama akaja mtu mwenye ukoma, akamsujudia akisema,

                  (a) Bwana ukitaka unaweza kunitakasa

                  (b) Bwana ukitaka waweza kunibariki

                  (c) Bwana ukitaka waweza kunihurumia

  10. (i) Taja jina la mfalme aliyemfunga na kumtia Yohana Mbatizaji gereza?

                  (a) Kayafa

                  (b) Rulea Sanga

                  (c) Mfalme Herode

    (ii) Kwani Yohana alifungwa gerezani?

                  (a)  Yohana alimwambia sio halali kwa Herode kuwa na nduguye       
                 Filipo awe mke wake na Herode.

                  (b) Yohana alimwambia sio halali kwa Kayafa kuwa na nduguye
                 Musa awe mke wake na Herode.

                  (c) Majibu ya hapo juu sio sahihi

    (iii) Kwanini mfalme alipoona watu akaogopa kumuua Yohana Mbatizaji?

                  (a)  Yohana alimwambia sio halali kwa Herode kuwa na nduguye
                 Filipo awe mke wake na Herode.

                  (b) Kwasababu watu walimuona Yohana Mbatizaji kama Nabii

                  (c) Kwasababu watu walimuona Yohana Mbatizaji kama Mfalme

    (iv) Ni nani aliyecheza mbele ya Herode wakati wa sikuku yake ya kuzaliwa akampendeza Herode kwa uchezaji wake?

                  (a) Binti Herode

                  (b) Mjukuu wa Herode

                  (c) Rafiki yake na Binti Herode

    (v) Ni nani alimshauri huyu mtu aliyecheza mbele ya mfalme Herode na mpaka Herode akakubali kutimiza kiapo chake cha kumpa chochote atakachoomba?

                  (a) mama yake

                  (b) Kaka yake

                  (c) Rafiki yake

    (vi) Huyo aliyemfurahisha Herode kwa kucheza aliomba  nini apewe na huyo mfalme?

                  (a) hakuomba chochote

                  (b) aliomba kichwa cha Yohana Mbatizaji katika mfuko

                  (c) aliomba kichwa cha Yohana Mbatizaji katika kombe

    (vii) Unafikiri Herode alifuarahia ilo ombi la huyu aliyecheza vizuri katika sikuku yake ya kuzaliwa? Na kama alifurahi au alisikitika ni kwanini?

                  (a) Herode alisikitika, kwasababu aliona ni aibu kwa watu waliokuwa
                 nao katika meza ya chakula na wote waliofika katika sikukuu yake

                  (b) Herode alisikitika, kwasababu aliona ni atakimbiwa na watu
                 waliokuwa nao katika meza ya chakula na wote waliofika katika
                 sikukuu yake

                  (c) Herode alisikitika, kwasababu aliona ni si haki na ni uonevu  kwa
                 watu waliokuwa nao katika meza ya chakula na wote waliofika katika             
                 sikukuu yake

    (viii) Baada ya kichwa cha Yohana Mbatizaji kukatwa na kukabidhiwa yule kijana alicheza vizuri mbele ya mfalme Herode, ni wapi alikipeleka hicho kichwa?

                  (a) mama yake

                  (b) Kaka yake

                  (c) Rafiki yake


Monday, July 9, 2012

SHETANI ANYOHANGAISHA MIOYO YA WANADAMU

Mwandishi: Rulea Sanga

Ndugu zangu nyakati hizi ni za kumtafuta Mungu na kufanya kazi ya Mungu. Ulimwengu umeharibika, taarifa za kutisha na za kukatishana tamaa zimezidi. Watu wanaishi maisha ya hofu, hawana amani ndani ya maisha yao. Ndoto za ajabu zimewatala, zinawafanya waishi maisha ya wasiwasi. Binadamu wamekuwa wanyama, hawana huruma na wanapenda kuona wenzao wanateseka.

Wengine hawapendi hata kuona mwenzao anafanikiwa, wako tayari kutumia njia zozote kuhakikisha mambo yako yanaharibika. Imani za kishirikina zimetawala, watu wanalogana, watu wako tayari kupoteza maisha ya wenzao ili mradi mambo yao yanasonga mbele. Ukipita mitaani utakutana na vichaa wanahangaika na wengine wako uchi- hakuna wa kuwasitiri. Watoto na watu wazima wanachukuliwa misukule, wanafanyiwa mambo ya ajabu huko misituni na wachawi, vyakula vyao ni vya ajabu. 
 
Kuna baadhi ya watu wamezuiliwa milango yao ya mafanikio na ndugu zao au jamaa zao. Kila unapojitahidi kufanya jambo fualni, halifanikiwi. Wengine wanajitahidi kusoma kwa bidii, lakini wanapokuja kufanya mitahini ya mwisho wanafeli, ila ukiangalia maendeleo yao kabla ya mitihani yalikuwa mazuri sana. Kuna wengine wamelogwa na kusemewa maneno mabaya na wabaya ya kuwa kila jambo utakalofanya hutafanikwa, nah ii imetawala sana katika kipindi hiki.

Wachawi wanawaloga watu na kuwatupia majini na kuwasemea maneno mabaya. Utaona msichana ni mrembo sana na amefanikiwa kimaisha lakini hapati mtu wa kumuoa. Wasichana kama hawa wanafikia hatua hata ya kuwa wabaya katika jamii na kuona kama wametengwa na ulimwengu. Wanatamani kufanya vitendo viovu na kudiriki kuingia katika ushiriana ili wapate waume. Na hili sio tu kwa wasichana bali hata kwa wanaume ambao nao hujiingiza katika mambo maovu ya ushoga, ushirikina, ulevi, utekaji, uchawi, wizi na mambo mengine kama hayo.

Barabarani lusambazwa nuksi za kila aina, ajali zimetawala. Wachawi wanaweka mambo yao ya ajabu katika barabara ili kusababisha ajali, na ajali inapotokea wao hufurahia kwani kwao damu ma myama ya watu ndio chakula chao kikuu na ndicho kinachowasaidia kufanikiwa mambo yao. Hili ni ja,bo la kusikitisha sana na linaumiza sana hasa pale unaposikia ndugu yako amepoteza maisha kwa jajali mbaya.

Vita ndani ya familia zimetawala sana katika ulimwengu huu, kuna baadhi ya familia hazielewani, utaona mama na mototo wake wanatukana na kushikiana visu ili wauane. Shetani ametawala katika familia zetu. Hapendi kuona wewe unaelewana na ndugu yako. Anajitahidi kutumia mbinu zake kuhakikisha hakuna amani katika familia yako. Cha kushangaza utaona pengine katika familia kuna wengine wamefanikiwa kiuchumi na nimatajiri sana, lakini ndani ya hiyo familia kuna maskini wakutupwa na hakuna wakuwasaidia. Shetani mara nyingine anaweza kukuzuia wewe kutokuwa na moyo wa kusaidia jamii yako, au anaweza kuzuia wewe maskini kuonekana hufai kwa yule ndugu yako aliyefanikiwa

Wasomi wengi wamesoma lakini wanakosa kazi, kila wakienda kuomba kazi hawafanikiwi. Kuna baadhi ya ofisi ukipeleka vyeti vyako na wakiona wewe umesoma sana wanakataa kukupa kazi eti kwasababu umesoma sana na hawataweza kukulipa mshahara kulingana na elimu yako. Shetani ni majanja sana na ni mjinga, huwapa wajiri kipofu cha kufikiri na kuwadanganya kwa kuwapa “statement” ambayo ni ya kipimbavu ya kuwafukuza wasomi wazuri ambao wangeweza kuinua kampuni. Baadhi ya wasomi wengine hawaangalii sana kiwango cha msharaha ila wanachotaka na “experience” tu ya kazi.

Shetani hana huruma kwa wanadamu, kuna baadhi ya watu wamelogwa kuwafanya mazezeta, wengine chakula chao ni mikaa ya moto, barafu, kinyesi, mikojo, michanga, kucha, na vitu ambavyo mwanadamu hawezi kuvila. Furaha yake ni kuona unateseka na hufanikiwi kwa lolote. 
 
Ombi langu kwako unayeteseka, jaribu kuwa karibu sana na Mungu kwa kufanya mapenzi yake mema. Pia kuwa na imani kwa kila jambo unaloomba kwa Mungu kuwa linaenda kufanyika. Kumkemea shetani kuwe ni moja ya kazi yako ya kila siku. Maombi yasipungue katika kinywa chako. Na unapoomba umaanishe na usiweke kama ratiba fulani. Maombi yako yawe silaha katika kupambana na adui shetani. Tafuta watu waliokoka kabisa na anza kushirikiana nao katika kusoma biblia na kuijadili ili kuwa na ufahamu wa kutosha kuhusiana na Mungu. Epukana na wanaokukatisha tamaa kuhusu Mungu. Ukiwa na Mungu utapambana na watu wengi ambayo watakukatisha tamaa, na huyo ni shetani kwani shetani mara zingine anatumia watu au rafiki au ndugu zako na kukuletea habari mbaya kuhusu Mungu.
 
Mungu wangu akubariki






Monday, July 2, 2012

PADRI AAMURU KABURI KUFUKIWA, AGOMA KUMZIKA MUFU KWA SABABU ALIACHA KUSALI

KATIKA hali isiyotarajiwa, Padri wa Kanisa Katholiki Jimbo la Sumbawanga , Evalin Kombe hivi karibuni aliamuru kufukiwa kwa kaburi lililokuwa tayari kuhifadhi mwili wa mmoja wa waumini wa kanisa hilo kwa dai kuwa muumini huyo alikuwa ameacha kusali.
Mbali ya kuacha kusali, Padri huyo pia alidai sababu nyingine ya kuzuia mwili wa marehemu usizikwe katika makaburi hayo, wakati wa uhai wake, alikuwa anaishi na mume bila kufunga ndoa kanisani.

Kitendo cha Padri huyo ambaye ni Paroko wa Kanisa la Pito lililopo kijijini kuzuia mwili wa marehemu Noelia Mwanisenga (29) asizikwe kwenye shamba hilo la wafu kulichelewesha maziko ya marehemu kwa zaidi ya saa tatu .
Akisimulia kisa hicho, mume wa marehemu Noelia, Boniface Sali (32), mkazi wa kijiji cha Tamasenga ambaye pia ni askari Mgambo alisema kuwa wakati wakijiandaa na maziko wachimba kaburi ghafla walirejea msibani Pito na kutoa taarifa kuwa Paroko ameamuru kaburi lifukiwe na kuwa marehemu wake hatazikwa katika shamba hilo la wafu.
Alisema baada ya majadiliano wafiwa walifikia uamuzi wa kuchimba kaburi jingine kijiji jirani cha Tamsenga na kumsitiri marehemu wao jioni tena bila ibada zinazohusu imani yake ya Kikatholiki aliyokufa nayo.

Sali alikiri kuwa yeye ni mlokole wa madhehebu ya Pentekoste na marehemu mkewe alikuwa muumini wa Kanisa Katholiki.
Ignas Mwanisenga ambaye alishiriki kuchimba kaburi la marehemu kijijini Pito anadai kuwa Padri Kombe alipofika makaburini alikuta wanamalizia kuchimba kaburi hilo na kuwataka kulifukia huku akiwatishia kuwa kama angekuwa na bunduki angeweza kuwaua.
“Alionekana kuwa na hasira kwani alitutishia kuwa kama angekuwa na bunduki angetuua, kwanza alifukia mwenyewe halafu alituachia sisi tutufukie kusimamia zoezi hilo mpaka tukalimaliza huku akisisitiza kuwa kama tungeshindwa angefukia yeye mwenyewe hata kama ingemchukua siku kadhaa kufanya hivyo” alisema Ignas .

Sali alisema yeye na mkewe ambaye alikuwa askari Mgambo waliishi pamoja kwa zaidi ya miaka minane na kujaliwa kupata watoto watatu na wiki mbili zilizopita aliaga dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu. Charles Kusula , Mjumbe wa Serikali ya Kijiji cha Tamasenga alithibitisha kuwa marehemu Noelia alizikwa kijijini humo saa 12 jioni .
Tukio hilo ambalo limetokea wiki mbili zilizopita, si la kwanza, kwani Padri huyo alishawahi kukataa kumzika katika makaburi hayo ya Pito, Marehemu Steven Kipesha (34), hali iliyomlazimu baba mdogo wa marehemu, Oto Kipesha mkazi wa Kijiji hicho cha Pito kumzika marehemu upenuni mwa nyumba yake.
Kutokana na kitendo cha Padri Kombe kufukia kaburi, ndugu wa karibu wa marehemu huyo na baadhi ya wakazi wa Kijiji cha Pito na vijiji jirani wamelielezea tukio hilo kuwa ni mkosi kwa wafiwa.
Baadhi ya wazee wa jadi waliozungumza na mwandishi wa habari hii wanadai kitendo cha Padri huyo kinaashiria mkosi kijijini humo wakisema kufukia kaburi tupu kutasababisha balaa jingine la kifo katika familia hiyo iliyozuiwa kumzika marehemu wao kaburini humo na kwenda kumzika kwingineko.

“Sisi katika desturi yetu ya kimila iwapo kaburi tayari limeshachimbwa lakini baadaye maamuzi yakatolewa marehemu asizikwe humo, basi hukatwa mgomba na ‘kuzikwa‘ kaburini , ikiwa ni njia ya kuondoa mkosi kwa wafiwa, lakini si kufukia kaburi likiwa tupu,” alisema mmoja wa wazee hao wa jadi ambaye hakuwa tayari jina lake liandikwe gazetini.
“Kwa kawaida tunavyofahamu sisi ni kwamba kama uamuzi umeshatolewa kuwa marehemu hatazikwa katika kaburi lililokwishaandaliwa kwa ajili yake basi kamwe kaburi hilo huwa halifukiwi, huachwa hivyo hivyo likiwa wazi na tupu lakini kitendo hiki cha Padri kufukia kaburi sio tu kimetustaajabisha wengi bali pia ni machukizo kwetu,” alisema Afred Mwananzumi , baba mdogo wa marehemu.

Naye mkazi mwingine wa kijiji hicho cha Pito Oto Kipesha alimweleza mwandishi wa habari hizi kijijini humo jana kuwa alifikia maamuzi ya kumzika Steven Kipesha (34) ambaye ni mtoto wa kaka yake upenuni mwa nyumba yao kijijini humo baada ya Padri Kombe kuwazuia wasimzike marehemu huyo katika shamba la wafu kijijini humo kwa madai kuwa aliacha kusali muda mrefu.
“Marehemu alihamia Tunduma miezi mitatu iliyopita na baadaye aliugua na kufariki dunia katika Hospitali ya Rufaa jijini Mbeya tulipopata taarifa za msiba tulijiandaa na kuusafirisha mwili hadi kijijini hapa lakini Paroko Kombe alituzuia tusimzike katika shamba la wafu kijijini hapa kwa kuwa eti alikuwa hasali …… mie nikachukua uamuzi wa kumzika upenuni mwa nyumba yangu.
Alipohojiwa na mwandishi wa habari hizi kuhusiana na visa hivyo viwili akiwa ofisini kwake jana katika Parokia ya Kanisa Katholiki kijijini Pito , Padri Kombe alikiri kuwa aliwaamuru vijana aliowakuta wakichimba kaburi katika shamba la wafu kijijini humo walifukie hata hivyo alikanusha kuwatolea maneno ya vitisho kuwa kama angekuwa na bunduki basi angewaua.
Akieleza sababu za kuchukua uamuzi wake huo , Padri Kombe alisema kuwa visa vya aina hiyo vimekuwa vikitokea sio kijijini humo pekee bali na kwingineko kwamba kidesturi zipo aina tatu za maziko katika Kanisa Katholiki ambapo marehemu wote wawili Kipesha na Noelia waliangukia katika aina ya tatu .
Alisema aina hiyo ya tatu inatokea pale muumini pamoja na kwamba amebatizwa, lakini hasali hivyo anajirudisha katika upagani basi azikwe mahali popote pale lakini sio katika shamba la wafu la Kanisa.

“Mara nyingi nimekuwa nikiwaeleza haya tena huwa nawafafanulia kuwa kwa kuwa hawataki kuja kanisani kusali basi wakifa wazikwe huko huko majumbani mwao kwa kuwa ni mahali wanapopapenda zaidi kwanini wasumbuliwe kupelekwa mahala pengine kwa maziko? “ Alihoji.
Pia aliendelea kufafanua akisema aina ya kwanza ya maziko inayofuatwa na Kanisa hilo Katholiki inahusu waumini waliobatizwa ambao katika uhai wao waliweza kutimiza na kuishi katika Ukatholiki wakisali na kushiriki mambo yote ya kanisa.
Padri Kombe alisema maamuzi hayo ya kutowazika katika shamba la wafu ni fundisho kwa wengine ili wafuate ibada kama watapenda kushughulikiwa kiimani baada ya kifo.

KAMA UNA MAONI YOYOTE NIANDIKIE HAPO CHINI AU TUMA UJUMBE KWENYE NO +255 715 033 671, +255 767 033 671 AU FB Martin Malecela follow me in Twetter martmalecela

Sunday, July 1, 2012

TUJIKUMBUSHE NA KILE KILICHOTUPIWA NA SAMSASALI KATIKA BLOG


Chini Ya Carpet......TB Joshua Kutua Tanzania??

Pichani ni Mtumishi wa Mungu kutoka Tanzania na kiongozi wa Kanisa la Ephata akiwa na Nabii TB Joshua nchini Nigeria mwaka 2009. Mtumishi Mwingira alifanya Ziara nchini humo na kuhudhuria Africa Apostoric Forum iliyofanyika nchini humo.


Baada ya Jitihada za Miaka ya Nyuma Kushindikana za Kumleta Mtumishi wa Mungu TB Joshua hapa Tanzania huenda mtumishi huyo akakanyaga ardhi ya Tanzania.


Chanzo Cha habari kilikataa kutaja nani na nani wanafanya mpango wa kumleta na lini na wapi ila alisema "Unakumbuka siku za nyuma ilikuwa Nabii TB Joshua aje na alisha ridhia mwaliko ule uliokuwa unaratibiwa na Mtumishi wa Mungu Apostle.............(Jina tunalo) na alishakubali ila Roho akaelekeza tofauti, basi mazungumzo yameanza tena, sababu imekuwa na support kubwa zaidi" mwisho wa kunukuu taarifa hiyo.


Blog ilipotaka kujua lini na wapi na nani ana organize chanzo kilisema "Mambo yakiwa tayari kila kitu kitakuwa hadharani"


NINI KIFANYIKE ILI KUDHIBITI UHARAMIA WA KAZI ZA WASANII NCHINI ILI KUHAKIKISHA WAHUSIKA WANAFIKISHWA KWENYE VYOMBO VYA SHERIA NA KUCHUKULIWA HATUA STAHIKI KAMA MAJAMBAZI WENGINE


Pamoja na serikali kuahidi kwamba juhudi zinachukuliwa ili kuleta heshima na thamani ya wasanii na kazi zao nchini, lakini kinyume chake hivi sasa kazi feki zimezagaa hadi vichochoroni.

Pamoja na wasanii kujinyima, kukopa, na kuangaika hapa na pale ili kuweza kuandaa kazi zao zinazogharimu mamilioni ya pesa lakini watu wanazitumia bila kutoa jasho lolote, tena wanaziuza bei chee. Hili ni janga, huu ni msiba mkubwa kwa wasanii nchini.

Uchunguzi uliofanywa kwa muda mrefu umebaini kuwapo kwa kundi kubwa la wafanyabiashara wanaouza kazi za Wasanii mbalimbali zilizodurufiwa (duplicated) kwa bei ya chini na kusababisha wasanii kutofaidika na kazi zao.

Nani awafute machozi wasanii, nani alete matumaini kwa wasanii? Nani atuondolee mtandao huu wa maharamia wa kazi za wasanii?

Ikiwa malaria haikubaliki, na uharamia huu haukubaliki.

Chama cha muziki wa injili nchini (CHAMUITA) kinapinga tabia hii
Kazi feki zikitayarishwa kuchomwa huko China

HERE IS THE AUTOBIOGRAPHY OF TB JOSHUA

(This man is real unique,i real admire his humility and true love-Author)


God chooses grace rather than works”(Ephesians 2:8-9)
This means that if the weak come to Him, He would help their weakness just as He would help the strong. God knows we are weak – that is why He chooses grace. If God had chosen works rather than grace, man would have the autonomy to choose whom to help with his works and how to do His works.
The battle would be for the strongest leaving no room for people like me (T.B. Joshua). The race would be for the swiftest leaving no room for people like me (T.B. Joshua).”
Isaiah 6:8 – “Then I heard the voice of the Lord saying, “Whom shall I send? And who will go for us?” And I said, “Here am I. Send me!”
T.B. Joshua is just one of those who have submitted to the will of God. He acknowledges that if God had chosen works rather than grace, no one would merit His mercy.
In a sermon titled, “By His Grace”, he explained:“Wisdom in the practical sense of ability and skill cannot guarantee success in life. It is the goodness of our cause that interests God more than physical and mental disposition. This explains why the weak people like me who are without great strength, a smooth tongue, fast legs or high learning should ever remain grateful to God”.
Right from the outset of his incredible journey, the hand of God has been clearly evident in the life of Prophet T.B. Joshua. He was born on June 12th, 1963 in the small village of Arigidi in Akoko, Ondo State, Nigeria. The pregnancy period of his mother was by no means ordinary, as the baby remained in her womb for 15 months before he was born. Significantly, almost a hundred years prior to his birth, it had been prophesied that a young man would emerge from the poor Oosin quarters and that God would use him mightily. Another remarkable event occurred when he was three days old, as a large boulder crashed through the roof of his house, missing the baby by mere inches. This incident led to his mother naming him, ‘Temitope’, meaning, ‘What You (God) have done for me is worthy of thanks’.
During his elementary education at St. Stephen’s Anglican primary school, Arigidi, he was the leader of the Student Christian fellowship. He was the smallest in the class but led the prayer during the school devotions and was known as ‘small pastor’. He was unable to complete his secondary education due to poverty.
Reflecting on his early life, he said: “I found myself in a family background that irritated me. My natural circumstance of birth was poverty. I come from a very humble background. Poverty loomed large in the family. The little education I had was through self-effort. I know many people with a similar circumstance of birth who did otherwise. They allowed their circumstance to influence their will. Their dreams crashed on the rocks of disappointment, failure and setback …In those early years of my life, we knew we would be blamed for what we gave our attention to.”
In an article written by T.B. Joshua himself, titled, ‘Everything Big Starts Little’, he explains more…
Very early in life, he knew how much he needed God, so he did not allow the situation around him to affect his relationship with God. As described in his own words, T.B. Joshua recounts how he discovered the direction of God’s calling for his life:

Sarah Shilla Kutoka na "Let It Rain, In His Presence"

Mwanamuziki anayekuja Juu katika Gospel Music, The Sarah Shilla siku ya Tarehe 5 August, 2012 Anatarajia ku "Launch" Albam Yake yenye Jina la "Let It Rain In His Presence"

Blog itazidi Kukupa Details za Tukio Zima Linavyokwenda.



Saturday, June 30, 2012

MCHUNGAJI BURTON SANGA ANAKUKARIBISHA KATIKA BLOG YAKE MPYA AMBAYO ITAKUWA INATOA HABARI ZA MUNGU NA MIKUTANO YAKE. KARIBUNI SANA WAPENDWA








WE ARE BUILT WITH THE WORD

Wise Man Harry gave an inspiring message to launch the service, titled, “Love Everyone, Trust Only God”.  He said that one of the great lessons life itself teaches us is that trust should not be readily given because we are in a danger zone where everyone lies to his neighbour. Great businesses do not just happen without trust; our greatest mistakes will happen because of quick trust. He said the same people who were praising Jesus were the ones who later crucified Him. Many times Jesus found Himself where people rejected Him because of His ideology.
He said we cannot succeed alone but we need good, inspired and informed people to succeed in life, which was why Jesus had 12 disciples. Those in whom we choose to trust should be led by God each day; when we trust them, we trust God.
TESTIMONIES

Healed Of Ovarian Cyst Through The Anointing Water
Mrs Ntisili Seng, a South African, was suffering from an ovarian cyst and had visited many gynaecologists for medical attention, who eventually recommended that she go for an operation. Her sister, in possession of the Anointing Water from The SCOAN rushed to her aid and  advised her to administer it in faith. To her surprise, the symptoms of the cyst disappeared and upon further medical examination, she was confirmed to be healed and without any trace of the ovarian cyst. Speaking to the congregation and viewers, she advised that people should not lose hope because God is always in control.

Healed Of Hypertension Through The Anointing Water
Mr Hassan Ola, from Warri, Delta State, had been suffering from hypertension for four years for which he could not get a solution. The heart disease had taken him to many places because it had deprived him of paying attention to his business, as he could not walk even for 30 minutes. He said he faced “troubles all over”.
He was lucky to obtain Anointing Water which God used to perform the divine miracle in his life. Today, he said, “I feel better. I can walk for more than one hour with no problem”. He said, “There is power in this water. You only need to believe.


Delivered From Fatal Accident Through The Anointing Water
Pastor Henry Neaba, based in Ebonyi State, Nigeria came to The SCOAN on January 2012 for “spiritual upliftment”. After receiving prayer from  Prophet T.B. Joshua, he returned home, believing that his case was settled. On March 12th, his boss had asked him to oversee a project at a site but felt strangely uneasy about the prospect. He decided to pray with Anointing Water in Jesus’ name to ward off the fear. He then boarded a okada (motorbike) to move to the site when, after five minutes, a car crashed into the bike. Pastor Henry flew off the motorbike, his head smashing into the windshield of the car. He went into a coma, his body slumped in a pool of blood. While in the coma, he saw himself on a spiritual journey which he could not understand but he kept shouting the name, Jesus. He saw a light and eventually saw T.B. Joshua who asked him to go back and pulled him to face where he was coming from.
Immediately he opened his eyes and slowly sat up to the amazement of the crowd of onlookers.  Unable to believe that he had survived such a traumatic accident, they rushed him to the hospital. When he was discharged, someone blessed him with a brand new car after hearing of surprising survival! He advised that people should believe in God as “any man who puts his trust in God will never be put in shame”.

Wednesday, June 27, 2012

MCHUNGAJI BURTON SANGA  NAPENDA KUWASHUKURU WOTE WALIHUSIKA KATIKA MSIBA WA MAMA YANGU MPENDWA AMBANGILE SANGA.

Shukrani zangu za dhati kwawale  wote waliokuwa pamoja nasi katika kumuuguza mama yangu alipokuwa hospitali ya Chimala Mbeya. Tunashukuru kwa kunifariji, kunichangia,kunitia moyo na maombi hasa pale mama alipokuwa amelazwa hospitalini.

Mbali na hapo ninawashukuru madaktari wote waliokuwa nami bega kwa bega kwa kumtibu mama yangu. Na pia namshukuru sana Dk. Mahenge kwa kujitoa nasi katika shughuli zote, tangia mama alipokuwa hospitalini mpaka anatoweka duniani. MUNGU AKUZIDISHIE PALE ULIPOTOA.

Napenda pia kutoa shukrani zangu za dhati kwa wote waliohudhuria katika mazishi ya mama yangu yaliyofanyika katika makaburi ya Itoroha Uyole Mbeya siku ya jumamosi 23 Juni 2012 pamoja na wachungaji wote, MUNGU WANGU NINAYEMTUMIKIA AWABARIKI.

Wenu katika Bwana
 MCH. BURTON SANGA


MSIBA ULIOMKUMBA BLOGGER WENU WA RUMAAFRICA, RULEA SANGA ALIPOFIWA NA MAMA YAKE MZAZI AMBANGILE LANZON SANGA
Hii ni siku ambayo siwezi kuisahau pale nilipompoteza mama yangu mzazi katika hospitali ya Chimala Mbeya siku ya ya Jumamosi 22 Juni 2012. Mama yangu alipata ugonjwa wa ghafla pale alipoaanza kutapika na baadae kukimbizwa dispensary na baada ya kupimwa aligundulika ana malaria mbili. Mama alirudishwa nyumbani na baada ya hapo usiku wake mama yangu hali iliaanza kubadilika na kuishiwa nguvu. Hali hiyo ilizidi kuwa mbaya na baadae kaka yangu Burton Sanga aliamua kukimbiza hospitali ya Chimala iliyoko Mbeya. Mama aliaendelea na matibabu na baadae kugundulika kuwa alikuwa na Blood Pressure (BP) na baada ya siku kama mbili aligundulika kuwa anaumwa Kisukari. Siku tatu baadae hali ya mama yangu ilikuwa mbaya sana.
Mama aliwekewa mpira ya Oxygen na mrija wa kupitisha chakula. Mama hakuweza kuongea kwa muda wote aliokuwa hospitali, lakini namshukuru sana Mungu wangu, baada ya kuniona mama alicheka kicheko cha maumivu na kuniambia "Mwanangu umekuja kuniuguza???" Nililia sana kumuona mama anavyoteseka na kuhema, kwani alikuwa anasumbuliwa sana na utoaji na uingizaji oxygen. Pia alikuwa analalamika na maumivu aliyokuwa anapata kutokana na kulalia mgongo kwa muda mrefu.
Siku ya Jumatano mama yangu hakuweza kuongea kitu chochote, macho yake yalikuwa yamefumba na mdomo wake ulikuwa umeachama kwaajili ya hewa. Mama alipochomwa na sindano na daktari kama nne begani hakuweza kushtuka wala kuhisi maumivu yote. Ndugu zangu walipokuwa wanatoa nguo zake mama alikuwa bado kafumba macho yake na hakuonyesha sign ya kuumia.
 
Nakumbuka kabla ya kifo cha mama yangu, ilikuwa ni siku ya Alhmaisi nilipomuombea sana mama yangu na kuwaaga baadhi ya ndugu zangu kuwa nataka niende Dar es Salaam kufuatilia pesa ambazo zitasaidia katika matibabu na siku ya jumatatu nitarudi tena Mbeya kuumuuguza mama yangu, lakini haikuwezekana. Ilipofika siku ya Ijumaa nilienda hospitalini kwaajili ya kumuaga mama yangu na ndugu zangu kuwa naenda Dar.
Nilipofika hospitalini nilikutana na shemeji yangu mke na kaka yangu Mchungaji Burton Sanga, alinikimbilia na kuniuliza "begi lako liko wapi?" na mimi nilimjibu "nimeliacha hotelini"  aliniangalia kwa huruma sana, na mimi nikaona baadhi ya ndugu zangu wako katika chumba cha kuhifadhia maiti. Shemeji aliniambia "Jipe moyo mama hayupo tena duniani" nililia sana kwa maana sikuamini kwani siku ya jana yake nilimuombea na kumshika mkono, kumbe ilikuwa ndio alama ya kuaagana 
Nilimshika mama yangu mkono kwa mara ya mwisho na usiku wa ijumaa mama aliaga dunia.
Siku ya Ijumaa ya 22 Juni 2012 mida ya saa 4:30am mama aliaga dunia, na sasa amepumzika katika makaburi yaliyoko Mbeya uyole kama unaelekea Tukuyu.
Mama ameacha watoto wanne, Yohana Sanga, Fidness Sanga, Burton Sanga na Rulea Sanga.
Blogger wenu nawaashukuru sana wale wote walionitumia pesa kwa kupitia Tigo Pesa kama rambirambi na maneno ya faraja ambayo yalinifariji sana. MUNGU WANGU ATAWALIPA
Ngoja tuone Safari nzima ilivyokuwa:

NIKIWA SAFARINI KUELEKEA MBEYA
 Nikiwa maeneo ya Morogoro
 Mishika ndicho kilikuwa chakula changu siku hiyo
Nikisubiri safari kuanza kuelekea Mbeya

MAMA AKIWA KATIKA HOSPITALI YA CHIMALA MBEYA
Mama yangu ambangile Lanzon Sanga akiwa amelazwa hospitalini Chimala Mbeya siku ya Jumamosi
 Kutoka kushoto ni wauguzi, dada yangu Aulelia Mahenge mtoto wa mama mkubwa, Binamu yangu, Mama Simda
 Shemeji yangu ambaye ni mke na kaka yangu Mchungaji Burton Sanga, Mama Judy.
Mama Judy amemlea mama yangu kwa muda wa miaka 17 tangia atoke Iringa na mpaka mauti imemchukua
Dada yangu Fidness Sanga akimwangalia mama 
 Blogger wenu Rulea Sanga (kulia) nikimtakia afya njema mama yangu

Daktari akimtibu mama yangu, pembeni ni shemeji yangu, mke na kaka yngu marehemu Amir Sanga a.k.a Short
 Daktari akiwa na baadhi ya ndugu na jamaa
PICHA BADO ZINAKUJA

Jifunze Kumiliki Majibu Ya Maombi Yako 2 -Mwl Sanga

Njia ya nne: Kumiliki muujiza kwa kuwatunza watumishi wa Mungu na kuchangia huduma mbalimbali.
Yoshua 12:1-3 kwenye ule mstari wa pili Biblia inasema “Basi wakamwandalia karamu huko naye Martha akamtumikia na Lazaro alikuwa mmoja wapo wa wale walioketi chakulani pamoja nao.
Hii pia ni habari nyingine inamhusu Lazaro ambaye Yesu alikuwa amemfufua baada ya kuwa amekufa kwa siku nne. Sasa Lazaro aliumiliki muujiza wake wa kufufuliwa kwa kumtunza Yesu pamoja na wanafunzi wake kumi na wawili. Hii ina maana Lazaro pamoja  na dada zake waliingia gharama kwa ajili ya kuwatunza Yesu pamoja na  wanafunzi wake, Kwa siku zote ambazo Yesu alikaa kwa Lazaro, Lazaro alihakikisha hawalali njaa, anawapa mahali pa kulala nk.


Sasa unaweza kumiliki muujiza wako kwa kuruhusu watumishi wa Mungu wakae nyumbani kwako. Huenda wamekuja kwenye mkutano au semina kwa wiki moja au mbili itoe nyumba yako itumike, kufanya hivyo ni kumfanya Mungu aendelee kukulinda wewe na yale aliyokupa maana anajua hutamnyima siku moja atakapohitaji kuvitumia. Wapo wengine wanaomiliki kwa kutoa magari yatumike kipindi chote cha mikutano, unaweza pia  kumiliki kwa kuchangia gharama za mikutano  si lazima pesa lakini hata kufanya kazi mbalimbali katika mkutano huo, huenda  ni  usafi,  kubeba vyombo, kufanya usafi walikofika watumishi, kuombea huo mkutano au semina nk. Nakuambia unaweza ukaona kama ni vitu vidogo lakini ndivyo mujibu ya maombi yanavyomilikiwa bila kujali Mungu amekutendea nini.

Nija ya tano: Kumiliki muujiza kwa kufanya  maamuzi ya kuokoka endapo Mungu alikufanyia huo muujiza kabla hujaokoka, na kuwaambia wengine habari ya Yesu aliyekuponya.

Ukisoma ile sura nzima ya 9 ya kitabu cha Yohana utakutana na habari ya kipofu mmoja tangu kuzaliwa kwake  ambaye Yesu alikuwa amemponya. Ule mstari wa 39 unasema “akasema,Naamini, Bwana akamsujudia” Ukisoma vizuri habari hii utagundua baada ya mahojiano marefu kati ya mafarisayo na yule kijana kuhusu uponyaji wake ndipo Yesu akamwuuliza je unamwamini mwana wa Mungu? Yule kijana akamwuliza ni nani huyo nipate kumwamini? Kwa kifupi Yesu akamjibu unayezungumza naye. Ndipo yule kijana  akasema, naamini Bwana akamsujudia.

Mtu mwingine ni Naamani ambaye tumekwisha ona habari zake, kitendo cha yeye kusema toka leo sitatoa sadaka kwa miungu  ya shamu ila kwa Bwana  ni dalili  ya kuonyesha kumwamini Mungu wa Israel. Hivyo hata leo wapo ambao Mungu anawatendea mambo mengi hata kabla hawajaokoka sasa ili kumiliki  hayo ambayo Mungu amekufanyia mwamini Yesu ndio huo muujiza utadumu. Wapo watu leo wanafunguliwa kwenye nguvu za mapepo huo ni  uponyaji. Sasa badala ya kuwasaidia watu wamwamini Yesu tunawaacha, nakuambia pepo watarudi kwa huyo mtu wenye nguvu zaidi kuliko yule wa kwanza.


Pia ukisoma vizuri habari hiyo hiyo utagundua kwamba huyu jamaa alimiliki uponyaji wake kwa kuwaambia wengine habari za Yesu na kukiri kwamba  mponyaji ni Yesu na si mtu mwingine, nakuambia  kufanya  hivyo ni kujihakikishia kudumu kwa huo muujiza na Mungu ataendelea kuutunza huo muujiza  maana wewe ni chombo chake. Mungu akikuponya au kukubariki usinyamaze kimya waambie wengine habari za Yesu aliyekuponya. Jifunze kutoka kwa mwanamke msamaria. Uponyaji wa nafsi yake ulipelekea watu wengi wa mji wa Samaria kuokoka. Soma kile kitabu cha Yohana sura ya nne mistari 30 ya kwanza utaiona habari hii.

Mpenzi msomaji wangu mpaka hapa naamini utakuwa umepata kitu cha kukusaidia labda nikuambie hivi  siri kubwa ya mafanikio ni kuliweka neno la Mungu kwenye matendo, si unajua imani pasipo matendo imekwisha kufa katika nafsi ya huyo mtu mwenye imani hiyo. Nimeamua  kuandika ujumbe  huu baada ya kuona wana wa Mungu wengi imefika mahali  wanakuta yale ambayo Mungu aliwapa kama majibu ya maombi yao yameshaharibiwa na shetani, wapo waliozaa watoto wao wakafa na walimuomba sana Mungu kuhusu hao watoto nk. Sasa  ni imani  yangu kwamba tangu sasa jambo lolote ambalo Mungu atakupa kama jibu la maombi yako utalimiliki.
Ndimi katika huduma

Mwl Patric Sanga

VANYASANGA POST TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...