Sunday, August 26, 2012

WAINJILISTI KUTOKA SCOAN KWA NABII T.B. JOSHUA KUINGIA TANZANIA

Mwandishi: Rulea Sanga

Watanzani tunaugeni mkubwa sana kutoka kwa Nabii TB Joshua. Hawa si wengine ni WAINJILISTI ambao wanakuja kutuhudumia Watanzania. Hii ni baraka tumepewa na Mungu kwa watu kama hawa kuingia nchini kwetu.

Tumekuwa tukiwaangalia katika Emmanuel TV kwa muda mrefu na tumekuwa tukitamani kuwaona uso kwa uso. Nisikuchoshe kwa maneno mengi mdau wangu, ngoja nikupe mchakato mzima 
Unatakiwa kufika Jumatatu 27.08.2012 saa moja katika ofisi za TB Joshua Dar es Salaam, na wale waliojiandikisha kwenda SCOAN Nigeria  waje pia na medical report zao eneo la Water Front jijini Dar es Salaam.
Wainjilisti watakutana na wale  waliojiandikisha kwenda SCOAN Nigeria siku ya Jumanne Diamond Jubilee.
Watanzania naomba tufike ili kupata ujumbe kutoka kwa watumishi wa Mungu. Mungu wangu awabariki.

Mimi kama blogger nawatia moyo kufika, kumbukeni na mimi nilipata muujiza wa kuonana na Nabii TB Joshua mwezi Aprili 2012


SCOAN-Nigeria

BBlogger Rulea Sanga nilipokuwa SCOAN Nigeriahttps://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh3g_1qEmAEtpb9iZ8V8tibGLVX9JLu3LGfaSB9NXxf6JvmJhVIeRrbEFmuLPqhA08D6YvqBGRnPiCXrYIUqq4w7GBWmW1XyTIgKNgqlYi3uCidF-CrGVfii9TGS9QMGDpMF1sQugrEuZ6T/s1600/five_wise_men_SCOAN.jpg
Wise Men

Ndani ya Sinagogi

Kwaya ya SCOAN

Watu wengi wamepona kwa kupitia Emmanuel TV hasa pale unapogusa mkono wa Nabii TB Joshua ambao huunyosha katika screen yako

No comments:

Post a Comment

VANYASANGA POST TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...